Permaculture

Permaculture ni mkusanyiko wa mbinu mbalimbali za maisha endelevu ambazo zinaongozwa na maadili matatu:

  1. Kutunza mazingira

  2. Kumjali mwenzako

  3. Kujali vizazi vijavyo

Permaculture kama mfumo ilianzishwa na Bw. Bill Mollison katika miaka ya themanini. Inaunganisha mafundisho ya kilimo endelevu, kusimamia na kutunza maji ya mvua, kuhifadhi mazingira, kutengeneza umeme kwa njia endelevu, kuimarisha jamii na uchumi kwa njia endelevu na kadhalika.

Mbinu zote kwa jumla zinajaribu kutekeleza malengo yafuatayo:

  1. Punguza matumizi ya rasilimali

  2. Tumia rasilimali ileile mara nyingi iwezekanavyo

  3. Tengeneza badala ya kununua tena

  4. Tafuta matumizi mapya kwa rasilimali badala ya kuichoma au kutupa tu.

Kwenye shamba letu tunatumia na kufundisha mbinu mbalimbali za permaculture ambazo zinalingana na imani yetu kwa Mwenyezi Mungu. kwa mfano:

  • Mifereji ya kukingia maji ya mvua

  • Choo cha kutengenezea mboji

  • Mfumo wa “aquaponics” (kufuga samaki pamoja na kuotesha mboga)

  • Kilimo cha mseto

  • Ufugaji endelevu

  • n.k.