Volunteers wapya wanakuja…
Wiki ijayo, wanajitolea (volontia) watatu vipya wanawasili shambani. Zaidi ya hayo, kuna familia kutoka Kenya itakayokaa nasi kwa mwezi mmoja kujifunza Kiswahili. Tunawatarajia kwa furaha kubwa! Ndiyo maana kwa sasa tuko kwenye shughuli nyingi za kutayarisha kila kitu ili wajisikie wakaribishwa na wakiwa nyumbani:
Kukagua vyumba kama kila kitu kipo na kununua mahitaji yote yanayotakiwa
Kutengeneza vitu vilivyoharibika
Kukagua, kusafisha, na ikibidi kutengeneza mabafu na vyoo
na kadhalika.
Katika wiki ya kwanza, wanajitolea watapata mafunzo ya utangulizi kuhusu utamaduni na maisha ya Kitanzania (ambayo ni tofauti sana na ya Kizungu), na jinsi ya kuishi vyema hapa. Baada ya hapo, watafanya kazi kwa muda katika nyanja zote za shamba ili waelewe jinsi kila kitu kinavyoendeshwa na kujipatia nafasi inayowafaa, kisha wataandika maelezo yao wenyewe ya kazi (job description) kwa ajili ya huduma yao.
Na baadaye, bila shaka watajitambulisha kwenu hapa kwenye tovuti hii.